Kuna nyimbo ukizisikiliza zinakubamba kwa muda mrefu! Unarudia kuusikiliza tena na tena — labda mashairi ndio yanakuvutia, midundo ya ala, mantiki ya wimbo n.k. Wakati mwingine inategemea unausikiliza ukiwa kwenye mawazo gani.
Show Love. Wimbo wa Nako 2 Nako. Ulinibamba. Kila kitu, kuanzia sekunde ya kwanza hadi sekunde ya mwisho. Sitaki kuuchambua leo, ila tulia kwanza halafu usikilize kwa makini:
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Sitaki kusema ubeti wa kwanza ni mkali kuliko nyingine; ila tegea sikio kitu ambacho G-Nako anasema kwenye ubeti wa kwanza.
Bila shaka sasa hivi unaelewa kwanini tumeamua kumpa nafasi ya kuhojiwa kwa njia ya simu na tovuti hii — kama msanii wa kwanza. Ilikuwa ngumu kumpata siku ya leo kutokana na harakati zake kibao. Lakini, bahati nzuri tukampata kabla giza halijaanza kuingia.

Ni maongezi mafupi tu ya kawaida. Tulikuwa tunataka kufahamu nini kinaendelea kwenye shughuli zake, mipango yake kimuziki na kutupa maelezo mafupi ya Hip Hop ni nini hasa. Wimbo “Show Love” ulibuma kwenye media; unataka kujua anasemaje kuhusu hili? Msikilize:
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Nadhani umemsikia mwenyewe. Tunapenda kumshukuru G-Nako (na Nako 2 Nako kwa ujumla) kwa kutupa muda wake na kubadilishana mawazo hapa na pale.
Tunasubiri wimbo wake mpya “Juu Ulipo” (aliyomshikirisha Joh Makini) na hiyo video ya “Show Love” ili tuifanyie kazi kidogo. Inapatikana Youtube, ila kuna kitu fundi mitambo wetu angependa kukifanya…
Bofya hapa ili uweze kusikiliza nyimbo nyingine za Nako 2 Nako.
Samahani kwa kwikwi za hapa na pale — kulikuwa na harakati nyingi nadhani, na kama unavyojua ni interview ya kwanza kwa njia ya simu!
Pamoja!
UPDATE!
Kama ambavyo G-Nako alivyotuahidi, ametutumia nyimbo yake mpya “Juu Ilipo” (ft. Joh Makini). Sikiliza jiwe:
Audio clip: Adobe Flash Player (version 9 or above) is required to play this audio clip. Download the latest version here. You also need to have JavaScript enabled in your browser.
Vunja mifupa kama meno ipo!




15 Comments
Asante mzee… Looking forward to more one on ones! Keep up the spirit.
Kwnn msipost hyo interview kwa kuandika kile mlichoongea hata kwa ufupi kuliko kuanza kusikiliza hayo maongezi.
@anon – asante, tutaandika hizi interview, au summary, in future. for this post tulikuwa na muda fupi ndio maana tukaamua kupost ile recording.
umeonaje lakini… je utapenda kusikia au kusoma “one on one” kama hii?
Me toka mwanzo nilikuwa naisapoti hii Web mliyoanzisha na ni Fan pia kwenye Fb page yenu(Raphamatic) mko poa nimependa ile review ya wimbo wa kikosi na mada nyingine ila unajua na2mia cmu so nimeshindwa kusikiliza hyo interview ya Huyo Professor ol in ol ningependa interview 2we 2nazisoma itakuwa fresh.na hata mkiacha link kama m2 atamind kusikiliza kwa mda wake.Big up
Asante sana mimi nimoja ya watu wanao mkubali gnako lakini ingependeza muwemna post kwanjia yamaandishi
Asante sana @Raphmatic. Lazima itarekebishwa. Tutaku-update soon…
oyo wadau …bana izo ishu z interview ha2zipat mana wabish 2na2mia phone inakua ngum ku browzz 2ngezipata kw maandish ingekua gud idea
ujumbe umefika @rygon. Hilo ni wazo zuri manake hatutaki mtu yeyote akose uhondo. Hivyo wazo lako litaanza kufanyiwa kazi kwenye interview inayofuata..stay tuned..asante kwa mchango wako.
Tuko pa1 wazee ktk kuliendeleza hil gurudumu la hip-hop 1 love
HIP HOP ni mzuka sana big up kwa NAKO 2 NAKO 2po pamoko sana ktk harakati za kuiendeleza hip hop R-CHUGA STAND UP,G NAKO MKALIIIIII! ARIFU FULL.
NI MZUKA SANA PANDE ZANGU NOW DAYZ GONGAMX NI MBINDE KUIPATA ILA BADO NADILI NAYO COZ KUPATA NYIMBO ZA KIBONGO NI NGUMU SANA…AM IN NORWAY BUT NI MZALIWA WA TANGA MJINI….TZ HIP HOP IN MA BLOOD……ONE LOVE ALL HIP HOP SURPPOTERS
Naipenda hip hop kutoka kwa N2N,RIVER CAMP,FID Q,wateule,watengwa¤ DislimiNATION
oi oi oi pamoja mwana……. big up wakali wa hiphop….. ningependa kujarib msikilize bt yang kama mtaipenda musing nayo…
sawa bro wemkali lakin lord nikwel kakamatwa
gnako we mkali